Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jamhuri kumbana Tido Mhando Oktoba 16
Habari Mchanganyiko

Jamhuri kumbana Tido Mhando Oktoba 16

Tido Mhando, aliyekuwa Mkurugenzi wa TBC
Spread the love

UPANDE wa Mashtaka katika kesi ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando kuanza kumuuliza maswali mtuhumiwa huyo ifikao Oktoba 16 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tarehe hiyo, upande wa Jamhuri utaanza kumuuliza maswali Tido dhidi ya utetezi wake alioutoa tarehe 20 Septemba 2018 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Kabla ya tarehe hiyo kupangwa, Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi aliiahirisha kesi hiyo ambayo ilitakiwa kuendelea leo, kufuatia Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Leonard Swai kupata udhuru.

Tido anayetuhumiwa kuisababishia serikali hasara ya Sh. 887.1 milioni kutokana na matumizi mabaya ya madaraka alipokuwa mkurugenzi wa TBC, alitakiwa kuulizwa maswali na upande wa jamhuri baada ya upande huo kufunga ushahidi baada ya mashahidi wake akiwemo Mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa, Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa TBC, Clement Mshana pamoja na Ofisa Uchunguzi wa TAKUKURU kutoa ushahidi wao kwenye kesi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!