Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jaji Warioba: Muwapishe wengine madarakani
Habari za Siasa

Jaji Warioba: Muwapishe wengine madarakani

Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba
Spread the love

JAJI Joseph Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu amewashauri viongozi wa umma kutokaa madarakani muda mrefu, akisema kwamba kitendo hicho hakina tija kwa masilahi ya taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Jaji Warioba ametoa ushauri huo leo tarehe 14 Oktoba 2019, wakati akizungumza katika Kongamano la Kumbukizi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, lililofanyika Wilaya ya Butiama mkoani Mara.

Jaji Warioba ameeleza kuwa, kitendo cha baadhi ya viongozi kukaa madarakani muda mrefu, kinasababisha ufanyaji kazi kwa mazoea, na kuathiri maendeleo ya nchi.

Na kushauri viongozi walioko madarakani muda mrefu, kuwapisha wengine.

“Usikae madarakani muda mrefu utakua na uzito wa kufanya kazi kwa wakati, utaanza kufanya kazi kwa mazoea. Kufanya kazi kwa mazoea haileti maendeleo, inatakiwa ifike mahali, unawapisha wnegine,” amesema Jaji Warioba.

Akizungumzia miaka 20 ya Tanzania bila ya Mwalimu Nyerere, Jaji Warioba amesema alikuwa anafuata sheria na kupenda ushauri kutoka kwa wengine.

“Nyerere alikuwa anapenda kufuata sheria, alikuwa mtu wa kawaida, wa kushaurika,” amesema Jaji Warioba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!