Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaji Mutunga wa Kenya azindua kitabu Tanzania
Habari Mchanganyiko

Jaji Mutunga wa Kenya azindua kitabu Tanzania

Jaji Mstaafu wa Kenya, Willy Mutunga (kulia) akizindua kitabu sambamba na Jaji Joseph Warioba na Jaji Mstaafu wa Tanzania, Othman Chande
Spread the love

 

JAJI Mkuu Mstaafu wa Kenya, Willy Mutunga amezindua kitabu chake alichokipa jina la ‘Beacons of Judiciary Transformation’ leo Ijumaa tarehe 29 Aprili 2022, jijini Dar es Salaam nchini Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Jaji Mutunga aliyehudumu kama Jaji Mkuu wa Kenya kwa miaka minne kuanzia 2010-2014, amezindua kitabu hicho chenye mchanganyiko wa hotuba zake, maamuzi yake na maandiko ya kitaalamu, kikiwa na kurasa 504.

Jaji huyo aliyeingia madarakani baada ya kuundwa kwa Katiba Mpya katika taifa hilo, amesema katika kitabu chake hicho ameandika hotuba zake 60, maamuzi saba ya kesi alizohukumu akiwa kama Jaji Mkuu na maandishi ya kitaalamu matatu.

 

Kiongozi huyo mstaafu amesema sababu za kuzindulia kitabu hicho nchini Tanzania ni kutokana na mapenzi yake ya Watanzania ikiwa pamoja na kusoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia mwaka 1968.

Hafla hizo ilihudhuliwa na wadau mbalimbali wa sheria nchini ikiwa Majaji waastaafu, majaji wa Mahakama ya Tanzania na mawakili mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!