Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jaji Mkuu, Spika Ndugai wampa kibarua mrithi wa Dk. Ndugulile
Habari za Siasa

Jaji Mkuu, Spika Ndugai wampa kibarua mrithi wa Dk. Ndugulile

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Ashatu Kijaji
Spread the love

 

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Ashatu Kijaji, amepewa kibarua cha kuziunganisha taasisi za Serikali na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA). Anaripoti Patricia Kighono, TUDARCo … (endelea).

Dk. Ashatu amekabidhiwa jukumu hilo leo Jumatatu, tarehe 13 Septemba 2021 na Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, pamoja na Spika wa Bunge, Job Ndugai, baada ya kuapishwa kuiongoza wizara hiyo, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Dk. Kijaji ameapishwa siku moja baada ya kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kuongoza wizara hiyo, akichukua mikoba ya Dk. Fuastine Ndugulile ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Juma, amemuomba Dk. Kijaji, aziunganishe mahakama katika mkongo wa taifa wa mawasiliano, ili ziende sambamba na mabadiliko ya TEHAMA.

“Pongezi nitoe kwa waziri wa TEHAMA ambayo sisi mahakama yangu namtegemea sana kutusaidia kuingia katika karne ya 21, ambayo rais umewahi kusema inasukumwa na mapinduzi ya nne ya viwanda. Tunategemea mkongo wa Taifa utaendelea kuunganishwa na mahakama zetu,” amesema Prof. Juma.

Aidha, Prof. Juma amemuomba Dk. Kijaji ashushe gharama za vifurushi vya intaneti, ili kurahisisha matumizi ya TEHAMA nchini.

“Gharama za internet zitashuka sababu hiyo ndiyo barabara iliyobaki kufikia mapinduzi ya nne ya viwanda,” amesema Prof. Juma.

Naye Spika Ndugai amemuomba Dk. Kijaji aziunganishe taasisi za Serikali na mifumo ya TEHAMA, ili kupunguza gharama zinazotumika katika kuchapisha ripoti na taarifa mbalimbali, ikiwemo za mabaraza ya madiwani.

Job Ndugai

“Kwenye teknolojia ya habari dunia ya sasa iko kwako, utusaidie sana kama alivyosema Jaji Mkuu, mabadiliko ya teknolojia ni muhimu katika maendeleo ya wananchi na hasa katika kupunguza gharama za Serikali,” amesema Spika Ndugai na kuongeza:

“Yako maeneo ya improvement mengi, ukitazama vile mabaraza ya madiwani yaliyotapakaa nchi nzima yanavyotumia makabrasha ya karatasi, tukiingia kwenye TEHAMA tutapunguza gharama kwa kiasi kikubwa sana, lakini hata vikao vya madiwani vitapungua,”

“Na katika maeneo mbalimbali ya utumishi na utoaji huduma, inakuwa bora zaidi kupunguza rushwa sababu mteja na mtoa huduma hawakutani uso kwa uso.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!