Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Jaji Mkuu Rasmi Kuanza Kazi
Habari Mchanganyiko

Jaji Mkuu Rasmi Kuanza Kazi

Jaji Mkuu wa Tanzania, Ibrahim Hamis Juma akila kiapo
Spread the love

Rais wa Tanzania  Dkt John Mgufuli, amemwapisha Jaji Mkuu wa Tanzania, Ibrahim Hamis Juma, ambapo awali alikuwa akikaimu nafasi alikuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, baada ya aliyekuwa Jaji Mkuu kustaafu kisheria, Mohamed Othman Chande, anaandika Irene david.

Akizungumza leo na waandishi wa habari katika shughuli za kuapishwa zilizofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, Jaji Ibrahim amesema ataendeleza misingi mizuri waliyoiacha majaji wakuu waliopita ikiwemo kupambana na rushwa katika taifa na pia kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa mahakama katika mikoa mbalimbali nchini.

Aidha ameongezea kwa kusema kuwa atasimamia haki kama sheria inavyoitaka Mahakama kutoa haki kwa raia wote nchini.

“Tatizo la uhaba wa mahakama ya mwanzo nchini imekuwa ni changamoto na kwamba tayari mikakati ilishawekwa na Jaji aliyepita hivyo kilichobaki ni utekelezaji na kuwa utafanikiwa mpango huo,” amesema Jaji Ibrahim.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!