Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaji Mkuu awataka mahakimu wajitenge na siasa
Habari MchanganyikoTangulizi

Jaji Mkuu awataka mahakimu wajitenge na siasa

Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma
Spread the love

 

JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, amewataka mahakimu wasijihusishe na masuala ya siasa, kwani yamepigwa marufuku na Ibara ya 113 A ya Katiba ya nchi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Prof. Juma ametoa wito huo leo Jumamosi, tarehe 16 Julai 2022, akiwaapisha mahakimu wakazi wapya 20, jijini Dar es Salaam.

“Naomba msome Ibara ya 113 A , ya katiba ambayo inasema itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama Kuu, Msajili wa Mahakama ngazi yoyote, hakimu wa ngazi yoyote kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa utabaki na haki ya kupiga kura. Hivyo lazima tuelewane,” amesema Prof. Juma.

Kiongozi huyo wa mahakama, amewataka watendaji wa mhimili huo wasifanye vitendo au kutoa kauli ambazo zinahusiana na masuala ya siasa.

“Usifanye mambo au kutoa kauli ambayo mwananchi anaweza kukuhusisha na chama chochote, sababu sio lazima uwe mwanachama inaweza kuwa vitendo vyako, maneno unayosema, nguo unazovaa zikahusishwa, kwa hiyo yote ni vizuri tujiadhari sana,” amesema Prof. Ibrahim.

Katika hatua nyingine, Prof. Juma amewataka mahakimu kutoahirisha kiholela tarehe za utoaji hukumu au uamuzi.

“Jambo lingine ambalo mahakimu wamekuwa wakilifanya ambalo wananchi wamekuwa wakilalamika, ni kupanga tarehe ya kusoma hukumu halafu inafika husomi. Unapanga tarehe nyingine, inafika husomi. Wananchi wanakuwa na haki ya kukushuku,” amesema Prof. Juma.

1 Comment

  • Duh!
    Mahakama zipi ziko chini yako?
    Mahakama za Ardhi zina kesi za kubambikiza za miaka zaidi ya 20. Hii inauwa uchumi wa wazawa.
    Unda tume ya majaji watatu wazifanyie kazi.
    Acheni kuendelea na kesi hizi zenye historia ya kufungw na kufungukiwa eti ni mpya. Lakini ugomvi unahusu ardhi hiyo hiyo kwa miaka mingi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!