Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaji Mkuu awapa angalizo watumishi wanaoihama Mahakama
Habari Mchanganyiko

Jaji Mkuu awapa angalizo watumishi wanaoihama Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma
Spread the love

 

JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, amewapa angalizo watumishi wa mahakama wanaohama kwa sababu ya maslahi, akisema siku maslahi ya mahakama yatakapoboreshwa wakitaka kurudi watakumbushwa kwamba walikimbia majukumu yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Prof. Juma ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 29 Juni 2022, akifungua mkutano wa tatu wa Baraza Kuu la Saba la Wafanyakazi wa Mahakama ya Tanzania, uliofanyika jijini Dodoma.

“Pamoja kwamba ni haki ya mtumishi kuhama taasisi ya umma kwa kufuata utaratibu, bado mimi nashangaa wanaofikiri kuondoka mahakama waende sehemu nyingine yenye maslahi mazuri kwa sababu naamini maslahi yetu yakishakuwa bora watatamani kurudi,” amesema Prof. Juma.

Prof. Juma amesema “tunaboresha, watakaoondoka mkirudi tutawakumbusha kwamba mlitukimbia.”

Mkuu huyo wa Mahakama ya Tanzania, amesema wanaofanya vitendo hivyo siyo watumishi bali ni wafanyakazi na kwamba wanachoangalia ni maslahi yao binafsi.

“Watu kama hao sio watumishi bali ni wafanyakazi na wanachoangalia zaidi maslahi yao binafsi, kwa hiyo tusiwe wafanyakazi tuwe watumishi ambao tunaangalia picha kubwa zaidi ambayo ni ustawi wa haki, utawala bora na sisi tunaamini tuna mchango mkubwa sana katika shughuli zetu za kila siku,”amesema Prof. Juma.

Prof. Juma amewataka watumishi wa mahakama kuwa wavumilivu wakati Serikali ikiboresha maslahi yao.

“Shughuli zetu hazilingani kabisa na malipo tunayopata, ukijilinganisha na wale waliopo sekta binafsi waliosoma kama ninyi wana malipo makubwa zaidi lakini sisi tunajivunia hiyo picha kubwa ya ustawi wa Watanzania wengi kuliko ustawi wa biashara zetu,” amesema Prof. Juma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!