Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jafo afurahishwa na maonyesho ya wanawake wafanyabiashara Dar
Habari Mchanganyiko

Jafo afurahishwa na maonyesho ya wanawake wafanyabiashara Dar

Spread the love

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Selemani Jafo amepongeza maonyesho ya wafanyabiashara wanawake yanayoendelea kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Waziri Jafo aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akifungua maonyesho hayo ambayo yanaendelea kwenye viwanja hivyo ambayo yanatarajiwa kufikia kilele siku ya Almahisi ijayo kwa wanawake mbalimbali kupewa tuzo.

Maonyesho hayo yameandaliwa na Chemba ya Wafanyabiashara Wanawake (TWCC) na kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani GIZ na wafadhili mbalimbali.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa maonyesho hayo jana jijini Dar es Salaam, Waziri Jafo alisema baada ya kutembelea mabanda mbalimbali amejionea bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wafanyabiashara wanawake ambazo nyingi zinaviwango vya kimataifa.

“Nimefarijika sana kuona bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na nyingi zina nembo ya ubora wa Shirika la Viwango TBS zinahadhi ya kuuzwa kwenye maduka mbalimbali makubwa hapa nchini mnastahili pongezi kubwa sana,” alisema

Alisema wanawake hao wameonyesha ujasiri wa hali ya juu kuanzisha vikundi vya uzalishaji bidhaa mbalimbali hali ambayo imechangia kuongezeka kwa nafasi za ajira kwa vijana, anawake na hata kwa wanaume wengi nchini.

Alisema pamoja na janga la ugonjwa wa COVID uchumi wa Tanzania umeendelea kufanya vizuri na wanawake wametoa mchango mkubwa sana kwenye kutengeneza fursa za ajira kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora wa kimataifa.

Alisema amefarijika sana kuona wanawake wakiwa kwenye vikundi mbalimbali vilivyopata mikopo ya asilimia 10 zinazotoka kwenye halmashauri mbalimbali na kufanikiwa kuanzisha biashara zao ambazo zinakwenda vizuri.

“Kuna mabanda nimepita wameniambia wanauza bidhaa ndani nan je ya nchi hongereni sana kwa hatua hii kubwa mliyopita mafanikio haya tuliyofikia ni sababu ya wanawake kuwa mahiri ya kurejesha mikopo kwa wakati,” alisema Waziri Jafo.

Alisema anatamani sana kuona bidhaa hizo zinasambazwa kwenye maduka yote makubwa hao nchini na zingine kusafirishwa nje ya nchi kwani zinasifa ya kuvuka mipaka ya Tanzania.

Aidha, Waziri Jafo aliwataka wanawake hao kutumia fursa ya ujenzi wa miradi mikubwa kama ule wa kuzalisha Megawati 2,150 wa Julius Nyerere kwenda kuuza bidhaa zao kwa watu wanaofanyakazi kwenye mradi huo.

“Wakina mama nawaomba sana msiwe wanyinge nyinyi ni mashujaa kwasababu nyinyi ndiyo mnajenga msingi wa nchi hii na mchango wenu kwenye maendeleo ya nchi ni mkubwa sana. Tuendelee kufanyakazi tumsaidie rais wetu kutimiza ndoto zake za kujenga uchumi imara,” alisema Jafo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!