Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jafo aeleza mikakati ya kuboresha mazingira Dodoma
Habari Mchanganyiko

Jafo aeleza mikakati ya kuboresha mazingira Dodoma

Spread the love

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dk. Selemani Jafo amesema ushirikishwaji wa wadau katika ngazi zote na matumizi bora ya maji ya mvua zinazoendelea kunyesha ni mojawapo ya mikakati endelevu ya kuigeuzia Dodoma kuwa ya kijani. Anaripoti Danson Kaijage,  Dodoma … (endelea)

Jafo ametoa kauli hiyo jana tarehe 26 Januari 2022 alipokutana na wadau wa mazingira wa Jiji la Dodoma kutoka sekta binafsi na taasisi za Serikali.

Mkutano huo ulilenga kuweka mikakati ya pamoja katika kutekeleza kwa vitendo kampeni ya kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.

“Zoezi la kuigeuza Dodoma ya kijani linaendelea kwa kupanda miti maeneo mbalimbali ya jiji la Dodoma ambapo zaidi ya miti 40,000 imeshapandwa katika maeneo ya viwanja vya Chuo kikuu cha Dodoma, Mji wa Serikali Mtumba, Eneo la Medeli na maeneo ya kuzunguka Shule za Msingi na Sekondari zilizopo Dodoma” Dk. Jafo alisisitiza.

Seleman Jafo

Pia ametoa wito kwa jamii kufuata taratibu na kuzingatia sheria na kuacha kujishughulisha na shughuli zisizoendelevu ikiwemo uchomaji wa moto hovyo katika maeneo mbalimbali, hususan maeneo ambayo miti inapandwa.

Naye Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Edward Nyamanga ametoa wito kwa sekta binafsi na wafanyabiashara wa aina mbalimbali Jijini Dodoma kushiriki kwa dhati katika kuunga mkono serikali kwenye azma yake ya kuifanya Dodoma kuwa Jiji la mfano nchini katika masuala ya Hifadhi na Usafi wa mazingira.

Amesema lengo la kuanzishwa mpango wa kupanda miti wa kulifanya jiji la Dodoma kuwa la kijani ni kuhakikisha kuwa maeneo ya wazi, pembezoni mwa barabara, makazi pamoja na maeneo ya kuzunguka mashamba yanapandwa miti ili kuhifadhi mazingira na kupendezesha jiji la Dodoma.

Kwa upande wake Meya wa Jiji la Dodoma Profesa Davis Mwamfupe amesema zoezi la upandaji miti liwe endelevu na kutoa rai kwa Serikali kuepuka zoezi la upandaji miti wakati wa maadhimisho na sherehe za kitaifa pekee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!