Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Jacob Zuma wa Afrika Kusini ajisalimisha gerezani
Kimataifa

Jacob Zuma wa Afrika Kusini ajisalimisha gerezani

Jacob Zuma
Spread the love

 

JACOB Zuma (79), Aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, ameanza kutumikia kifungo cha miezi 15 gerezani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ni baada ya Mahakama nchini humo, Jumanne ya tarehe 29 Juni 2021, kumhukumu kifungo hicho, baada ya kumtia hatiani kwa kukaidi agizo la kufika mahakamani kuhudhulia kesi inayomkabili ya ufisadi wakati alipokuwa rais.

Baada ya umuauzi huo, wafuasi wake walizunguka makazi yake wakizuia asikamatwe, jambo lililowafanya ujumbe wa polisi kufika nyumbani kwake, Jimbo la Kwazulu Natala.

Katika mazungumzo yao, walikubaliana kwamba Zuma ajisalimishe yeye mwenyewe na alitii wito huo na jana Jumatano, tarehe 7 Julai 2021, akisindikizwa na walinzi wake, alikwenda katika gereza lililokaribu na nyumbani kwake.

Polisi nchini humo wamethibitisha Zuma kujisalimisha huku baadhi ya wafuasi wake, waliokuwa wamekusanyika nyumbani kwake, wakionesha kutofurahishwa kwa kiongozi huyo wa zamani wa Afrika Kusini, kuhukumiwa kifungo gerezani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!