Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Jacob Zuma aachiliwa kwa dhamana
Kimataifa

Jacob Zuma aachiliwa kwa dhamana

Jacob Zuma
Spread the love

 

RAIS wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ameachiliwa kwa dhamana katika gereza la Estcourt mashariki mwa nchi hiyo kutokana na sababu za kiafya hazikuelezwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mamlaka ya magereza nchini humo ilitangaza tarehe 5 Septemba, 2021 kuwa kiongozi huyo amelazwa hospitalini kwa muda wa mwezi mmoja sasa.

Zuma (79), amekuwa akitumikia kifungo cha miezi 15 jela kwa kudharau mahakama tangu Julai mwaka huu, baada ya kukataa kufika mbele ya tume inayochunguza ufisadi chini ya utawala wake.

Kwa mujibu wa mamlaka ya magereza, uamuzi huo umechukuliwa baada ya kupokea ripoti ya matibabu yake.

Zuma pia anashtakiwa katika kesi ya ‘Thales’, kesi nyingine ya ufisadi iliyoanzia mwishoni mwa miaka ya 1990.

Wakati kesi yake imepangwa kuanza tena Alhamisi wiki hii, Zuma amekataa kuendelea kuchunguzwa ilihali sasa amelazwa hospitalini.

Kufungwa kwake kulisababisha ghasia kadhaa na visa vya uporaji nchini humo hali ambayo ilisababisha vifo vya zaidi ya watu 350 mwezi Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!