Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Israel yaanza mashambulizi Gaza
Kimataifa

Israel yaanza mashambulizi Gaza

Spread the love

 

JESHI la Israel limefanya mashambulizi ya kijeshi baada ya kudai, Palestina kushambuliwa nchi hiyo kwa maguruneti. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Jeshi hilo limeeleza, limelenga kundi la waasi la Hamas ambao ni chama tawala cha siasa cha Palestina, na kwamba mashambulizi hayo yamelenga kambi mbili za ‘waasi’ hao.

Israel imeeleza, mashambulizi ya Palestina katika ardhi ya Israel, hayajasababisha madhara yoyote.

Hamas imeeleza, pamoja na mashambulizi ya Israel kuendelea, eneo la Gaza litaendelea kupiginiwa na Wapalestina mpaka mwisho wa uhai wao, akisistiza nchi hiyo haijafanya mashambulizi Israel.

Israel imeweka vikwazo mbalimbali vya kuingia Palestina kupitia barabara, baharini pamoja na viwanja vya ndege. Mgogoro wa ardhi kati ya Israel na Palestina ulianza mwaka 1967.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!