Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Iran yagomea vikwazo vya Marekani
Kimataifa

Iran yagomea vikwazo vya Marekani

Rais wa Iran, Hassan Rouhani na Donald Trump wa Marekani
Spread the love

RAIS wa Iran, Hassan Rouhani ameahidi kupinga vikwazo vya Marekani dhidi ya taifa lake, vinavyotarajiwa kuanza kutekelezwa leo tarehe 5 Novemba 2018. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mwishoni mwa wiki iliyopita Marekani ilitangaza kuibua vikwazo vya zamani na kuanzisha vikwazo vipya dhidi ya Iran, huku vikwazo hivyo vikilenga sekta ya taasisi za kifedha, mafuta, gesi, usafirishaji wa majini.

Akihutubia baraza la mawaziri la Iran leo Jumatatu, Rais Rouhani amesema Iran imetengeza sera za kufuta vikwazo vya Marekani.

Amelitaka baraza hilo kuhakikisha kwamba Marekani inaelewa kwa lugha rahisi kwamba, hawawezi kushughulika na taifa lao kwa kutumia nguvu, shinikizo na vikwazo.

Rouhani amejigamba kuwa, kitendo cha Marekani kuziondoa nchi nane zinazonunua mafuta ya Iran katika vikwazo vyake, ni ushindi kwa taifa lake.

“Jamhuri ya Kiislam ya Iran inaweza kuuza mafuta yake hata kama nchi nane hazijaondolewa kwenye vikwazo,” amesema Rouhani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!