Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Inonga akabadhiwa Tuzo na Emirates mchezaji bora Aprili
HabariMichezo

Inonga akabadhiwa Tuzo na Emirates mchezaji bora Aprili

Spread the love

 

Mlinzi wa kati wa klabu ya Simba, Henock Inonga amekabidhiwa tuzo ya mchezaji bora wa mashabiki (Emirate Aluminium Simba ACP Fans Player of the Month) kwa mwezi Aprili 2022, mara baada ya kuwashinda Shomary Kapombe na Josh Onyango. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea.

Mchezaji huyo amekabidhiwa tuzo hiyo hii leo tarehe 7 Mei 2022, kwenye makao makuu makuu ya kampuni ya Emirates Aluminiun Sinza jijini Dar es Salaam.

Beki huyo ambaye amekuwa na kiwango bora hivi karibuni aliibuka kidedea mara baada ya kupata kura 2277 sawa na asilimia 82.14, huku akifuatiwa na Kapombe aliyepata kura 457 sawa na asilimia 16.49 na wa mwisho ni Onyango aliyepata kura 38 sawa na asilimia 1.37.

Ndani ya mwezi Aprili, Inonga amecheza mechi nne sawa na dakika 360 huku akionyesha kiwango safi kwenye michezo yote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!