Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ingizeni wake zenu – Zungu
Habari za Siasa

Ingizeni wake zenu – Zungu

Mussa Zungu, Mbunge wa Ilala
Spread the love

MUSSA Zungu, Mbunge wa Ilala, amewataka maofisa na askari magereza kulinda heshima ya nyumba za serikali waliokabidhiwa, kwa kuhakikisha wanaingiza wake zao. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya majengo 12 ya nyumba za askari hao zilizoko Ukonga, jijini Dar es Salaam leo tarehe 23 Januari 2020, Zungu amewataka kuingiza wake zao kwenye nyumba hizo.

Zungu amesema, nyumba hizo zimeombewa dua na mashekhe, mapadri pamoja na maaskofu, hivyo wanatakiwa kuwa waadilifu katika matumizi ya nyumba hizo.

“Nyumba hizi zimeombewa dua na masheikh na baba paroko. Na mtu atakayeingia kwenye nyumba hizi, dua hii ina maana muwe waadilifu. Mkiingia humu ndani ingizeni wake zenu ili kuwe na heshima kwa aliyejenga aliyetoa pesa na heshima ya kiti cha uraisi,” amesema Zungu.

Majengo hayo  anayokabidhiwa Rais John Magufuli,  majengo manne ni ya maafisa wa jeshi la magereza na nane kwa ajili ya maaskari wa kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!