Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro kutimua Polisi wabambika kesi
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro kutimua Polisi wabambika kesi

Simon Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP)
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amewaonya askari polisi kuacha tabia ya kuwabambikia wananchi kesi huku akiahidi kwatimua kazi watakaobainika kufanya hivyo, anaandika Mwandishi Wetu.

IGP Sirro alisema askari wa aina hiyo ndiyo anaowatafuta na kwamba akiwabaini atawatimua kazi ili kuhakikisha jeshi la polisi linaaminika katika jamii nzima.

Sirro alitoa kauli hiyo alipotoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari baada ya kumaliza shughuli zilizokuwa zimepangwa na jeshi hilo kanda maalum Tarime na Rorya.

Sirro ameonya kwamba askari wa namna hiyo hawatakiwa na kwamba kila mtumishi wa jeshi hilo lazima awe na weledi.

Amewataka wananchi watakaokumbwa na tatizo hilo kutoa taarifa kwa maofisa wa jeshi hilo ili kuwabaini wale wanaoendekeza tabia hiyo.

”Hizi habari za baadhi ya askari polisi kuendekeza tabia ya kuwabambikia kesi wananchi zinasikika mitaani, hebu wale wanye shida hiyo wawaoneni na kutoa taarifa kwa maafisa wa polisi na kamanda wa kanda maalum Tarime na Rorya ili sisi tuweze kuwashughulikia vilivyo askari polisi wa namna hiyo” alisema Sirro.

Katika hatua nyingine IGP Sirro aliwaondoa hofu waandishi wa habari kwamba watakuwa salama wanapokuwa wanafanya kazi na jeshi hilo na kuwataka kulinda maadili ya kazi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!