Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro awaonya polisi kutoingilia NEC
Habari za Siasa

IGP Sirro awaonya polisi kutoingilia NEC

IGP Simon Sirro
Spread the love

INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro amesema, Polisi hawahusiki kutangaza mshindi wa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 bali kazi hiyo inafanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

IGP Sirro ametoa kauli hiyo baada ya kuwapo kwa video inayozunguka mitandaoni ikionyesha Kamanda wa Polisi Wilaya ya Hai (OCD) Mkoa wa Kilimanjaro akimweleza Freeman Mbowe, mgombea ubunge wa Hai kwamba hatoshinda kwenye uchaguzi huo.

Katika video hiyo, inamwonyesha Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema akizungumza na OCD huyo aliyemwomba afanye mkutano huku OCD huyo akimtaka kuondoka akisema “panda kwenye gari uondoke, wewe utamshinda huyo, huwezi kumshinda hata ufanyaje, yaani kwenye mawazo yako (Mbowe) unawadanganya watu kwamba utamshinda, huwezi kumshinda hata ufanyaje.”

OCD wa Hai akizungumza na mgombea ubunge wa Hai kupitia Chadema, Freeman Mbowe

Kutokana na hilo, IGP Sirro amesema, timu kutoka makao makuu imekwenda kuchunguza hilo tukio kuona kuna nini, “suala la majibu kwamba utashinda au utashindwa siyo kazi polisi hata siku moja ni kazi ya tume.”

“Kwa hiyo tunachunguza kuona kuna jambo lina ukweli kutokana na ile ‘clip’ tutachukua hatua dhidi ya huyo ofisa. Niwahakikishe Watanzani kwamba tunachunguza,” amesema IGP Sirro

Amesema, jeshi la polisi lina taratibu zake ambazo askari wote wanapaswa kuzifuata “na polisi anakwenda tofauti na miongozi, tunamwajibusha kwa mujibu wa taratibu zetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!