Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro aita ndugu kuchukua mwili wa Hamza, atoa ujumbe
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro aita ndugu kuchukua mwili wa Hamza, atoa ujumbe

Hamza Mohamed, aliyefyatulia risasi Polisi na kuwaua
Spread the love

 

INSPEKTA Jenerali wa Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amesema mwili wa Hamza Mohamed ambaye aliwaua watu wanne wakiwemo askari polisi watatu, utakabidhiwa kwa ndugu zake au utazikwa na halmashauri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Tukio hilo lilitokea tarehe 25 Agosti 2021 katika makutano ya barabara ya Kinondoni na Kenyatta karibu na Ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam.

Hamza anadaiwa kuua askari polisi kwa Bastola aliyokuwa nayo kisha akachukua silaha walizokuwa nazo na kuanza kufyatua risasi hovyo na kumuua mlinzi wa kampuni ya ulinzi ya SGA, Joseph Okotya Mpondo.

Askari polisi waliouawa ni; Miraji Khatib Tsingay, Emmanuel Keralya na Kangae Jackson ambao miili yote minne iliagwa jana Ijumaa, tarehe 27 Agosti 2021, katika viwanja vya Kurasini Polisi kisha kusafirishwa kila mmoja kwenda kuzikwa kwao.

Leo Jumamosi, IGP Sirro akizungumza jijini Dar es Salaam amesema, mwili wa Hamza wataukabidhi kwa ndugu zao kama watachelewa halmashauri watauzika huku akiwataka Watanzania kujifunza kwa kile alichokifanya kijana huyo.

“Mwili wa Hamza tutawakabidhi ndugu zake, kwani tayari sisi tumekwisha ufanyia kazi, lakini siku zikipita hawajaja kuuchukua halmashauri itakwenda kuuzika,” amesema

“Hiyo familia inajisikiaje, hiyo familia ya Hamza inajisikiaje, fikiria wewe ndiyo mama yake, baba yake, kuzaa kwake imetuletea baala Watanzania. Niwaombe Watanzania wengine wasituzalie watoto kama Hamza,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!