Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro abadili bosi wa trafiki, apangua Ma-RPC
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro abadili bosi wa trafiki, apangua Ma-RPC

IGP Simon Sirro
Spread the love

INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro amefanya mabadiliko ya baadhi ya makamanda wa polisi wa mikoa (RPC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Katika mabadiliko hayo, IGP Sirro amembadilisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa kuwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani (trafiki) kuchukua nafasi ya Fortunatus Musilim ambaye anakwenda kuchukua nafasi ya Mutafungwa.

Taarifa iliyotolewa jana Alhamisi tarehe 3 Desemba 2020 na Msemaji wa Polisi Tanzania, David Misime ilielezea mabadiliko hayo ni ya kawaida.

Misime alisema, licha ya nchi kuwa shwari, polisi linaendelea na operesheni mbalimbali zikiwepo za kukamata wanaojihusisha na uharifu mbalimbali ikiwemo wanaojihusisha na dawa za kulevya na matukio ya unyang’anyi na uvunjifu wa majumba

Mabadiliko ya makamanda yanahusisha, aliyekuwa RPC wa Kinondoni, Edward Bukombe amehamishiwa makao makuu kitengo cha picha na video na nafasi yake imechukuliwa na Ramadhan Kingai ambaye awali alikuwa Mkuu wa Upelelezi (RCO) Mkoa wa Arusha.

Wilbroad Mutafungwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro

Aliyekuwa RPC wa Lindi, Stanley Kulyamo amehamishiwa Shule ya Polisi Moshi kuwa Afisa Mnadhimu wa Chuo hicho na nafasi yake imechukuliwa na Mtatiro Kitinkwi ambaye awali, alikuwa Afisa Mnadhimu Shule ya Polisi Moshi.

Aliyekuwa RPC wa Tabora, Barnabas Mwakalukwa amehamishiwa makao makuu kuwa Afisa Mnadhimu katika Kamisheni ya Ushirikishwaji wa Jamii na nafasi imechukuliwa na Safia Omary Shomari ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu namna moja makao makuu.

IGP Sirro amemhamisha Lucas Mkondya kutoka Idara ya Maendeleo na Milki makao makuu kuwa Kaimu Kamishna wa Fedha na Lojistiki na nafasi yake kuchukuliwa na John Gudaba.

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime

Katika mabadiliko hayo, Mpinga Gyuumi amehamishwa kutoka kitengo cha Ufuatiliaji na Tathimini makao makuu ya polisi Zanzibar kuwa mkuu wa utawala na rasilimali watu makao makuu Zanzibar.

Aliyekuwa mkuu wa utawala nma rasilimali watu , Faustine Shilogile amehamishiwa kuwa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) makao makuu ya Polisi Dodoma, kuchukua nafasi ya Charles Kenyella ambaye amestaafu utumishi wa jeshi la polisi kwa mujibu wa sharia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!