Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Idadi ya vifo tetemeko la ardhi yafikia 9000
Kimataifa

Idadi ya vifo tetemeko la ardhi yafikia 9000

Spread the love

 

IDADI ya vifo vilivyotokana na tetemeko la ardhi lililotokea Jumatatu wiki hii nchini Syria na Uturuki vimefikia 9,000. Inaripoti Mitandao ya Kijamii … (endelea).

Timu za waokoaji katika nchi hizo nchi ziliendelea kuwatafuta manusura waliofukiwa kwenye vifusi vya majengo yaliyoangushwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyozikumba nchi hizo.

Zaidi ya mitetemeko 20 kati ya hiyo ilikuwa na kipimo cha 4.0 au zaidi, na kutikisa eneo lililo kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili.

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tedros Ghebreyesus ameelezea kuwa pamoja na wananchi wa Uturuki na Syria katika kipindi hiki cha huzuni mkubwa.

Amesema idadi ya vifo haizingatii huzuni na hasara zinazopitia familia hivi sasa ambazo zimepoteza baba, mama, binti, mtoto chini ya vifusi, au ambazo hazijui kama wapendwa wao wako hai au wamekufa.

Akizungumza kwenye mkutano wa WHO mjini Geneva, Tedros amesema shirika hilo linatuma ndege za kukodi na vifaa vya matibabu kwa nchi zote mbili na kwamba litafanya kazi kuwasaidia watakapopata afueni na kujenga upya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

error: Content is protected !!