Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Idadi ya vifo tetemeko la ardhi yafikia 9000
Kimataifa

Idadi ya vifo tetemeko la ardhi yafikia 9000

Spread the love

 

IDADI ya vifo vilivyotokana na tetemeko la ardhi lililotokea Jumatatu wiki hii nchini Syria na Uturuki vimefikia 9,000. Inaripoti Mitandao ya Kijamii … (endelea).

Timu za waokoaji katika nchi hizo nchi ziliendelea kuwatafuta manusura waliofukiwa kwenye vifusi vya majengo yaliyoangushwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyozikumba nchi hizo.

Zaidi ya mitetemeko 20 kati ya hiyo ilikuwa na kipimo cha 4.0 au zaidi, na kutikisa eneo lililo kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili.

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tedros Ghebreyesus ameelezea kuwa pamoja na wananchi wa Uturuki na Syria katika kipindi hiki cha huzuni mkubwa.

Amesema idadi ya vifo haizingatii huzuni na hasara zinazopitia familia hivi sasa ambazo zimepoteza baba, mama, binti, mtoto chini ya vifusi, au ambazo hazijui kama wapendwa wao wako hai au wamekufa.

Akizungumza kwenye mkutano wa WHO mjini Geneva, Tedros amesema shirika hilo linatuma ndege za kukodi na vifaa vya matibabu kwa nchi zote mbili na kwamba litafanya kazi kuwasaidia watakapopata afueni na kujenga upya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!