Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa ICC yatoa hati ya kukamatwa kwa rais Vladmir Putin wa Urusi
Kimataifa

ICC yatoa hati ya kukamatwa kwa rais Vladmir Putin wa Urusi

Rais wa Urusi, Vladimir Putin
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Kimataifa ya Uhalifu wa kivita (ICC) imetoa hati ya kukamatwa kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin. Vinaripoti Vyombo vya Habari vya Kimataifa …(endelea).

ICC inadai kuwa kiongozi huyo anahusika na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na kuwahamisha watoto kutoka Ukraine kwenda Urusi kinyume cha sheria.

Inasema uhalifu huo ulifanyika nchini Ukraine kuanzia tarehe 24 Februari 2022 – wakati Urusi ilipoanzisha uvamizi wake kamili.

Moscow imekanusha madai ya uhalifu wa kivita wakati wa uvamizi huo.

Mahakama ya ICC imemshtaki Putin kwa kuhusika katika kuwafukuza watoto, na inasema ina sababu za kuridhisha kuamini kuwa alifanya vitendo hivyo moja kwa moja, pamoja na kufanya kazi na wengine.

Aidha, Mahakama pia ilisema kiongozi huyo wa Urusi alishindwa kutekeleza haki yake kuwazuia wengine waliowahamisha watoto.

Kamishna wa haki za watoto wa Urusi, Maria Alekseevna Lvova-Belova, pia anasakwa na mahakama hiyo.

Hata hivyo, kibali hicho cha kumkamata putin na Bi Lvova-Belova kutolewa, ICC haina mamlaka ya kuwakamata washukiwa, na inaweza tu kutumia mamlaka ndani ya nchi ambazo zimesaini makubaliano yaliyounda mahakama hiyo.

Urusi sio mwanachama wa makubaliano hayo – kwa hivyo hakuna uwezekano wa kiongozi huyo kuwasilishwa mbele ya mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Xi Jinping awasili Urusi, kufanya mazungumzo na Putin

Spread the love  RAIS wa uchini Xi Jinping amewasili sasa nchini Urusi,...

Kimataifa

Maandamano Kenya, Afrika Kusini yashika kasi, wapinzani wakishikiliwa

Spread the love  MAANDAMANO ya kupinga serikali zilizoko madarakani nchini Kenya na...

Kimataifa

Maandamano Afrika Kusini: Tanzania yatahadharisha raia wake

Spread the love  WAKATI maandamano yaliyoitishwa na Chama cha upinzani Afrika Kusini,...

Kimataifa

Puto la kijasusi la China halikuleta tishio la usalama Marekani, lilifichua udhaifu wa ulinzi

Spread the love  PUTO la kijasusi la China limetajwa kuwa halikuweza kusababisha...

error: Content is protected !!