Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Huyu ndiye kiongozi mkuu wa Taliban aliye-mafichoni
Kimataifa

Huyu ndiye kiongozi mkuu wa Taliban aliye-mafichoni

Haibatullah Akhundzada
Spread the love

 

TANGU wachukue madaraka nchini Afghanistan tarehe 15, Agosti mwaka huu, viongozi kadhaa wa kundi la wanamgambo wa Taliban wameonekana hadharani mjini Kabul. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hata hivyo, mmoja wao ambaye ni kiongozi wao mkuu wa kundi hilo, Haibatullah Akhundzada ameendelea kusalia mafichoni.

Jana tarehe 29 Agosti, 2021 wasemaji wa Taliban walisema kuwa Haibatullah Akhundzada yuko katika mji wa Kandahar.

“Amekuwa akiishi hapo tangu mwanzo,” amesema msemaji wa Taliban Zabihullah Mujahid wakati Naibu wake amesema kwa upande wake kwamba kiongozi huyo ataonekana hadharani hivi karibuni.

Haibatullah Akhundzada, mtaalam wa masuala ya kisheria na kidini, alitangazwa mwezi Mei 2016 kuwa kiongozi wa Taliban, kundi ambalo wakati huo lilikuwa limekubwa na malumbano ya ndani.

Aliteuliwa siku chache baada ya kifo cha mtangulizi wake, Mansour, aliyeuawa na shambulio la ndege isiyo na rubani ya Marekani huko Pakistan, kwa lengo kuu la kuunganisha tena Taliban.

Kundi hili liligawanyika kufuatia mapambano ya kuwania madaraka baada ya kifo cha Mansour na siri waliokuwa wameficha kwa miaka mingi kuhusiana na mwanzilishi wao, Mullah Omar.

Taliban ilitoa picha tu moja ya Haibatullah Akhundzada na hadi sasa hajawahi kuonekana hadharani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!