HUKUMU ya kesi ya Jinai Na. 36/2020, inayomkabili kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mdude Nyagali, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, inatolewa leo Jumatatu, tarehe 28 Juni 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).
Hukumu hiyo ilipangwa kusomwa Jumatatu ya tarehe 14 Juni 2021, mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer, lakini iliahirishwa.
Hakimu Laizer alisema, ameahirisha kusoma hukumu hiyo, kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake.
Wakili wa Mdude, Faraji Mangula, alisema hukumu hiyo haikusomwa kwa kuwa haikuwa tayari.
Kada huyo wa Chadema anayesota rumande tangu Mei 2020, anakabiliwa na shtaka la kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin, zenye uzito wa gramu 23.4.
Mdude alikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, tarehe 10 Mei 2021, baada ya kufanyiwa upekuzi katika hoteli moja jijini humo, alikokuwa amepanga, na kudaiwa kukutwa na dawa hizo
Leave a comment