MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imeahirisha kutoa hukumu ya kesi namba 458 ya mwaka 2016 inayomkabili Mkurugenzi wa Jamii Forums, Maxence Melo na mwenzake ya kuzuiya Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).
Leo Ijumaa tarehe 30 Oktoba 2020, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Huruma Shaidi, amesema hukumu ya kesi hiyo haijawa tayari hivyo amepanga 17 Novemba 2020 ndio siku ya kutoa hukumu juu ya shauri hilo.
Mshitakiwa mwengine kwenye shauri hilo ni Mwanahisa mwenzake, Melo Mike Mushi ambaye wameshtakiwa pamoja.
Kwenye shauri hilo, mabosi hao wa Jamii forums wanashitakiwa kuendesha Mtandao wa Jamii Forum bila kutumia kikoa cha Tanzania mathalan;-www.habari.tz).
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuzuia jeshi la Polisi kufanya uchunguzi, kinyume na Sheria Namba 22 (2) cha Sheria ya Makosa ya Mtandano Namba 14 ya mwaka 2015.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo, kati ya Aprili Mosi, 2016 na 13 Desemba 2016 katika maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Leave a comment