Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Huduma ya luku majanga, Tanesco yaomba radhi
Habari Mchanganyiko

Huduma ya luku majanga, Tanesco yaomba radhi

Spread the love

 

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema, huduma ya manunuzi ya luku kwa njia ya mtandao, inatarajia kurejea leo Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021, kuanzia saa 12:00 jioni. Anaripoti Jemima Samwel, DMC…(endelea).

Ni baada ya kuadimika kwa saa kadhaa na kusababisha usumbufu kwa wananchi wanaotafuta huduma hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Tanesco imesema, kukosekana kwa huduma hiyo ni “hitilafu iliyobainika wakati wa maboresho yanayoendelea katika mfumo wa manunuzi ya Luku.”

“Tanesco linawaomba radhi wateja wake kutokana na kukosekana huduma ya manunuzi ya umeme wa Luku kwa njia ya mtandao. Huduma hiyo, inatarajia kurejea leo Jumatatu, kuanzia saa 12:00 jioni,” imeeleza taarifa hiyo

Hii ni mara ya pili ndani ya kipindi cha mwezi mmoja, tatizo hilo linajitokeza na kusababisha baadhi ya mameneja wa kitengo hicho, kusimamishwa kupisha uchunguzi.

Waliosimamishwa kupisha uchunguzi ni; Meneja wa Tehama na Huduma za Biashara wa Tanesco, Lonus Feruzi na wasaidizi wake wawili, Frank Mushi na Idda Njau.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!