Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Hizi hapa sababu za watoto kutoathirika na Korona
Afya

Hizi hapa sababu za watoto kutoathirika na Korona

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Said (kulia)
Spread the love

 

MKURUGENZI wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Said, amesema watoto wadogo hawaathiriki sana na Ugonjwa wa Korona (UVIKO-19), kwa sababu wamepewa chanjo nyingi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kanali Said amesema hayo leo Jumamosi, tarehe 7 Agosti 2021, akifungua warsha ya kuwajengea uwezo watetezi wa haki za binadamu, katika kukabiliana na maafa na majanga, mkoani Dar es Salaam, iliyoandaliwa na Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC).

Mkurugenzi huyo wa maafa amesema, mtoto hadi anafikisha umri wa miaka mitano, anakuwa amepata chanjo za aina tisa, ambazo zinamsaidia kutengeneza kinga za kukabiliana na magonjwa ikiwemo UVIKO-19.

“Wenzetu kina mama wakienda kujifungua wanapiga chanjo nyingi sana na watoto wakifika miaka mitano inatakiwa wapate chanjo tisa,  ndiyo maana wana immunite (kinga) sana. Korona inaweza ikampata asitingishike. Atashika nini lakini mikono iko salama. Sababu amechanjwa chanjo ya kutosha,” amesema Kanali Said.

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Said

Kanali Saidi amesema, watu wazima kuanzia miaka 40 na kuendelea, wako katika hatari ya kuathirika na ugonjwa huo, kwa kuwa kinga zao za utotoni zinakuwa zimeisha nguvu.

“Kuanzia miaka 40 kwenda juu huko, wako katika hatari sababu chanjo ulizopata zimeisha nguvu,” amesema Kanali Said.

Kanali Said amewaomba Watanzania wapate chanjo ya ugonjwa wa Korona, ili wajikinge na maambukizi yake.

“Wimbi la sasa sio kama la mwanzo,  ukasikia mtu anapiga chafya unamkwepa. Sasa hivi unaweza tembea kumbe una Korona, hujisikii kifua wala kukoa lakini wadudu unao wanaingia aidha kwa kutumia mdomo au kupumua hata kwa macho. Wakiingia wanapita kwenye mdomo na koo, wanajijenga wanashuka kwenye mapafu. Kwa nini usubiri mpaka ufike kote? Pata chanjo,” amesema Kanali Said.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!