Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hiki ndicho kilichowakwamisha Mbowe na wenzake
Habari za SiasaTangulizi

Hiki ndicho kilichowakwamisha Mbowe na wenzake

Spread the love

VIONGOZI wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wanaendelea kusota rumande kwa hoja kwamba, wanaweza kuhatarisha usalama wa jamii. Anaandika Faki Sosi…(endelea).

Hoja hiyo imewasilishwa jana na mawakiwa wa Jamhuri mbele ya Hakimu Mkazi Wilbard Mashauri wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam dhidi ya viongozi wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema; Vincent Mashinji, Katibu Mkuu; John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Bara; Salumu Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar; Easter Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini; Pater Msigwa, Mbunge Iringa Mjini walifikishwa katika Mahakama ya Kisutu jana kwa madai ya kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji Tanzania (NIT), Akwilina Akwiline na kurudishwa rumande.

Madai mengine ni pamoja na kuendelea kufanya mkusanyiko usio halali, uchochezi na kusababisha chuki katika jamii, uchochezi wa uasi, pia ushawishi wa utendekaji wa kosa la jinai.

Hatua ya kunyimwa dhamana kwa viongozi hao kumesababisha kuendelea kukaa mahabusu kwa siku mbili.

Hatua hiyo imetokana na mawakili hao wa serikali kuwasilisha hoja kwamba, wakiachwa kwa dhamana, watuhumiwa hao wanaweza kuhatarisha usalama wa jamii.

Hata hivyo, pingamizi hilo lilipingwa na jopo la mawakili wa utetezi liliongongozwa na Mwanasheria mwandamizi wa Chadema, Pater Kibatala.

Hakimu Wilbard alisikiliza hoja za pande zote mbili kwenye kesi hiyo ambapo alisema kuwa, atatoa uamuzi wa kupewa dhamana au kutopewa kwa watuhumiwa hao kesho Machi 29 mwaka huu.

“Kifungu cha 392 (A) cha mwenendo wa makosa ya jinai kinaturuhusu kuomba kuzuiliwa kwa dhamana ya washtakiwa kwa kuzingatia maslahi ya jamii na haki zao,” alisema Dk. Zainabu Mango, Wakili wa Serikali na kuongeza;

“Dhamana ni haki yao lakini hakuna haki isiyokuwa na wajibu, kila mtu anawajibu wa kutii sheria za nchi kutumi haki ya mtu mmoja kunapaswa kuzingatie haki za watu wengine.”

Amedai kuwa, makosa wanayoshtakiwa nayo viongozi hao yanaweza kuhatarisha usalama wa jamii na taifa kwa ujumla na kwamba, kupewa kwao dhamana kunaweza kuhatarisha usalama wa umma wa Tanzania.

Wakili huyo amedai kwamba, kupewa dhamana viongozi hao kunaweza kusababisha hatari ya kuendelea kufanya makosa kama hayo.

Faraja Nchimbi ambaye pia ni Wakili wa Serikali alisema, matamshi yaliyotolewa na viongozi hao yalisikika na yanaendelea kusikika ambapo yanaweza kuhatarisha amani.

Nchimbi amedai kuwa, zipo taarifa za kiupelelezi kuwa, matamko ya viongozi hao yamesababisha kutekelezwa kwa matukio ya uhalifu.

Wakili Kibatala anayetetea watuhumiwa ameieleza Mahakama kuwa, hakuna hoja ya kisheria kutoka kwa mawakili wa serikali inayoweza kuzuia dhamana za watuhumiwa.

Kibatala amakitaja kifungu cha 148 (5) cha mwenendo wa makosa ya jinai kinachoweka mipaka ya dhamana kwa mtuhumiwa na hakisemi kuhusu suala la usalama wa jamii.

“Kitu pekee kinachoweza kuzuia dhamana ni usalama wa mtuhumiwa ambapo sijamsikia mwasheria yeyote wa serikali akidai,” alisema Kibatala.

Amedai kuwa, kifungu hiko kinaitaka mahakama kujua kama kweli mtuhumiwa usalama wake upo mashakani. Amehoji kwanini Jeshi la Polisi liisukumie mahakama mzigo wake kwa kutaka liwafunge watuhumiwa kwa kulinda usalama wa jamii ilhali wanalipwa mishahara kwa kodi za wananchi ili kulinda usalama wao?

“Hakuna nyaraka yoyote hapa mahakamani inayofanya mahakama ifanye ulinganifu wa maslahi ya umma na washtakiwa.

“Hakuna wakili yoyote wa serikali aliyejitolea kuieleza Mahakama kwamba tangu Frebeuari 16 watuhumiwa walikuwa wapi na walifanya nini kinachohatarisha usalama wa jamii?” alihoji Kibatala.

Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo ambapo aliahidi kutoa uamuzi wa pingamizi hilo la serikali Machi 29 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!