Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Hichilema kama Nyerere: Atinga Marekani na msafara wa watu 3, apiga teke ndege ya rais
KimataifaTangulizi

Hichilema kama Nyerere: Atinga Marekani na msafara wa watu 3, apiga teke ndege ya rais

Spread the love

 

ANAFUATA nyayo za Hayati Mwalimu Nyerere? Ndilo swali linaloibuka miongoni mwa Watanzania baada ya Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema kuelekea nchini Marekani kwa kutumia ndege abiria badala ya ndege binafsi ya rais huku akiwa ameambatana na msafara wa watu watatu pekee. Anaripoti Helena Mkonyi, TUDARCo … (endelea).

Hichilema amesafiri jana tarehe 19 Septemba kuelekea jijini New York kushiriki mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN) unaotarajiwa kufanyika tarehe 23 Septemba 2021.

Neno moja kuu alilolitoa kuhusu safari yake, Hichilema ambaye amepanda ndege ya Shirika la Ndege la Qatar amesema mpangilio wa safari yake umelenga kubana matumizi.

“Tunakwenda New York kushiriki Mkutano Mkuu wa UN, tunakwenda kushirikiana na wadau mbalimbali na muhimu kwa faida ya nchi yetu. Tumekwenda ujumbe wa watu wachache ili kazi hii iwe na tija na gharama nafuu zaidi kwa taifa letu,” amesema.

Kauli hiyo imeibua mjadala katika mitandao ya kijamii huku baadhi ya wachangiaji wakimpongeza kwa hatua hiyo hasa ikizingatiwa nchi hiyo deni la zaidi ya Dola za Marekani bilioni 12.

Ikumbukwe kuwa Rais wa Kwanza na Baba wa Taifa Mwalimu, Julius Nyerere ni mmoja wa marais wanaoheshimika kwa kubana matumizi na kuacha kutapanya pesa.

Katika kipindi cha uongozi wake alikuwa anahudhuria mikutano ya aina hiyo kwa ndege za kawaida huku akiwa na msafara wa watu wachache.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

error: Content is protected !!