Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Hekari 2.8 Mil za misitu hatarini kupotea ifikapo 2030
Habari Mchanganyiko

Hekari 2.8 Mil za misitu hatarini kupotea ifikapo 2030

Spread the love

HEKARI za misitu zaidi ya 2.8 Milioni ziko hatarini kupotea ifikapo mwaka 2030, kutokana na ongezeko la matumizi ya nishati mbadala. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Hayo amesema Dk. Medard Kalemani, Waziri wa Nishati wakati akihutubia katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa uzalishaji umeme katika mto Rufiji ‘Stigler’s Gorge, leo tarehe 26 Julai 2019.

Dk. Medard amesema hekta za misitu laki 8 hukatwa kila mwaka kwa ajili ya matumizi ya nishati mbadala. Ambapo asilimia 71.2 ya Watanzania wanatumia mkaa na kuni huku Jiji la Dar es Salaam likiongoza kwa matumizi hayo, kwa kutumia magunia laki 5 kwa mwezi.

“Kila mwaka hekta laki 8 hukatwa kwa ajili ya matumizi ya nishati mbadala, tukiendelee mwaka 2030 hekari  2.8 milioni zitakatwa kwa sababu ya nishati jadidifu.

Kwa Dar es Salaam pekee, magunia laki 5 hupelekwa na kutumika kila mwezi, watanzania asilimia 71.2 wanatumia nishati mbadala ya kuni na mkaa,” amesema Dk. Kalemani.

Dk. Kalemani amesema mradi wa umeme wa Stiglier’s Gorge utasaidia kupunguza athari za uharibifu wa mazingira, ikiwemo kupungua matumizi ya nishati ya kuni na mkaa, na kutokomeza changamoto za ukataji wa misitu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!