Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Hekaheka DRC, uchaguzi njia panda
Kimataifa

Hekaheka DRC, uchaguzi njia panda

Spread the love

UCHAGUZI Mkuu katika Taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) upo njia panda baada ya mamlaka za nchi hiyo kujiumauma. Vinaripoti vyombo vya kimataifa … (endelea).

Uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Jumapili wiki hii ambapo sasa kauli zinazotolewa na mamlaka za DRC zinajielekeza katika kuahirisha uchaguzi huo licha ya kauli ya awali kudai kuwa, uchaguzi ungefanywa ndani ya muda uliopangwa.

Ceni Jean-Pierre Kalamba ambaye ni msemaji wa tume ya uchaguzi nchini humo ameeleza kuwa, hakuna uwezekano wa uchaguzi huo kufanyika Jumapili ya wiki hii kama ulivyopangwa.

Kauli yake ni tofauti na ile ya kwanza iliyotolewa wiki iliyopita baada ya ghala la kuhifadhia vifaa vya uchaguzi liliopo jijini Kinshasa kuungua na kuteketeza vifaa hivyo kwamba, uchaguzi usingeahirishwa.

Kauli iliyotolewa jana Jumatano inaeleza kuwa, maandalizi bado ni hafifu na hayajakamilika kutokana na tukio la uunguaji ghala hilo. Hata hivyo leo ilitarajiwa serikali kutoa msimamo wake kuhusu uchaguzi huo.

Ni zaidi ya miaka miwili sasa uchaguzi wa DRC umekuwa ukisogezwa mbele kutokana na Rais Joseph Kabila kung’ang’ania madaraka kwa kutoa visingizio mbalimbali.

Unyanyapaa wa viongozi wa upinzani DRC unaendelea kufanyika ambapo polisi nchini humo wamemzuia mmoja wa wagombea wakuu wa upinzani wa kiti cha urais, Martin Fayulu kuzindua kampeni zake katika mji mkuu wa nchi hiyo.

Tayari kuna tangazo la kupiga marufuku ya mikutano ya kisiasa ambapo Gavana wa Mji wa Kinshasa, Andre Kimpita, alisema kuwa hatua hiyo ya kupiga marufuku mikutano ya siasa imechukuliwa kwa sababu za kiusalama. Hatua hiyo imekasirisha zaidi wapinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!