Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Haya ni maajabu yake Mungu  
Kimataifa

Haya ni maajabu yake Mungu  

Hao siyo marais wa Korea Kaskazini wala Ufilipino, bali ni Cresencio Extreme (kulia) anayefanana na Rais Durtete wakati Howard X anafanana na Rais Kim.
Spread the love

AMA kwa hakika duniani ni wawili wawili. Hivi ndivyo unavyoweza kusema pale utakapokutana na Cresencio Extreme pia Howard X kwenye mitaa ya Hong Kong. Vinaripoti vyombo vya kimataifa … (endelea). 

Watu hawa wawili wamekuwa wakitikisa mitaa ya Hong Kong kutokana na namna walivyofanana na viongozi watata duniani Rodrigo Durtete, Rais wa Ufilipino na Kim Jong Un, Kiongozi wa Korea Kaskazini.

Kama utakutana na Cresencio Extreme pia Howard X mtaani, unaweza kustaajabu kuwa, imekuwaje Durtete na Kim wanatembe barabarani bila ulinzi wowote?

Watu wawili kila waliopata kuwaona, hushtuka na kudhani ni viongozi halisi kutokana na kufanana kwao.

Wamekuwa wakila pamoja, wakizungumza na kupiga picha pamoja pia wakivaa mavazi na mikato ya nywele inayoendana na viongozi halisi wa mataifa hayo mawili.

Cresencio Extreme ndiye anayefanana na Durtete wakati Howard X anafanana na Kim.

Hata walipohudhuria ibada ya Jumapili katika Kanisa la St. Joseph wakiwa na mavazi yale yanayopendwa kuvaliwa na viongozi hao halisi, walishangaza wengi.

Wakiwa mtaana viongozi hao feki walibeba bunduki na kuziinua juu wakiamini wanawasilisha hisia za viongozi wa wa mataifa hayo halisi ambapo Durtete anakabiliwa na shinikizo la kujiuzulu wakati Kim akipambana na Marekani kuhusu silaha zake za nyuklia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!