Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hatimaye Lema awasili Tanzania, akabidhiwa biblia na wazee wa Chadema
Habari za Siasa

Hatimaye Lema awasili Tanzania, akabidhiwa biblia na wazee wa Chadema

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema, amewasili nchini akitokea Canada, alikokuwa akiishi tangu 2020 baada ya kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa mwaka huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Lema amewasili Tanzania mchana wa leo tarehe 1 Machi 2023, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambapo anatarajiwa kusafiri hadi jijini Arusha, kwa ajili ya kushiriki mkutano wa hadhara wa Chadema.

Mwanasiasa huyo machachari nchini, amepokewa na umati wa watu waliofika uwanjani hapo, ambao walikuwa wamevaa sare za Chadema.

Baada ya kuwasili uwanjani hapo baadhi ya wazee ambao ni wafuasi wa Chadema, walimkabidhi biblia ya lugha ya kimachame, kama ishara ya kumpokea.

Mwakilishi wa wazee hao alimkabidhi biblia hiyo, huku akimkaribisha nyumbani baada ya kuishi ughaibuni nchini Canada kwa miaka zaidi ya miwili.

Lema ni miongoni mwa wanasiasa wa Tanzania waliokimbia nchi baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2020, kwa madai ya kupokea vitisho vya kiusalama. Viongozi wengine waliokimbia nchi kwa madai hayo walikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na Ezekiel Wenje na wote wamerejea Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!