Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Hasira za Simba, Yanga zahamia SportPesa
Michezo

Hasira za Simba, Yanga zahamia SportPesa

Spread the love

BAADA ya timu zote mbili kupoteza michezo yao siku ya Jumamosi wakiwa ugenini, zote zimerudi jijini Dar es Salaam kujiandaa na michuano ya kombe la SportPesa inayotarajia kuanza kutimua vumbi siku ya kesho 22 Januari, 2019 katika uwanja wa Taifa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea).

Yanga ilipoteza mchezo kwa mara ya kwanza kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara mbele ya Stand United ‘Chama la Wana’ baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0, huku Simba wakipokea kipigo kizito cha bao 5-0 kutoka kwa AS Vital ya Congo katika mchezo wa klabu bingwa barani Afrika hatua ya makundi.

Wawakilishi haio wa Tanzania wanatarajia kuanza kutupa karata zao siku ya kesho ambapo Yanga atamenyana dhidi ya KK Sharks kutoka nchini Kenya majira ya saa 10 jioni, huku Simba watashuka dimbani siku ya Jumatano kuwakabili AFC Leopards kutoka Kenya.

Ikumbukwe bingwa wa michuano hiyo atapata zawadi ya fedha, kombe sambamba na kucheza na klabu ya Everton inayoshiriki Ligi Kuu England kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa mashindano.

Timu zingine zitakazo shiriki michuano hiyo ni pamoja na bingwa mtetezi wa michuano hiyo mara mbili Gol Mahia kutoka Kenya, Bandari FC na Singida United ya Tanzania, Mbao FC ya Tanzania na Kaliabangi ya Kenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!