MKURUGENZI wa lebo ya Konde Gang, Rajabu Abdul ‘Harmonize’ hivi karibuni aliweka ratiba ya shoo zake nyingi za nchini Marekani, Bara la Ulaya na Afrika na hatimaye alfajiri ya leo tarehe 3 Septemba 2021 ameondoka Bongo kibabe akiwa na timu yake. Anaripoti Noela Shila, TUDARCo … (endelea).
Katika safari hiyo, Harmonize aliyeambatana na msanii wake Ibraah wameahidi kwenda kuitikisa Marekani.
Mbali na Ibraah, pia Harmonize ameambatana na meneja wake, Mjerumani na DJ wake, DJ Seven, tayari kabisa kwa ajili ya kwenda kukiwasha kwenye ziara hiyo ndefu.
Harmonize atafanya shoo Ohio, Huston, Phoenex, Las Vegas, New York, Edmondton, Los Angeles, Atlanta, Denmark, Swiden, Sierra Leone na kwingineko.
Leave a comment