Saturday , 10 June 2023
Home Kitengo Michezo Hans Poppe aongezwa kwenye kesi ya Aveva, Kaburu
MichezoTangulizi

Hans Poppe aongezwa kwenye kesi ya Aveva, Kaburu

Zakaria Hans Poppe
Spread the love

MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope, ameongezwa katika kesi ya tuhuma za kughushi nyaraka na kujipatia fedha inayowakabili Rais wa klabu hiyo, Evans Aveva na Makamu wa wake, Godfrey Nyange ‘Kaburu’. Anaripoti Jabir Idrissa … (endelea).

Waendesha mashtaka leo wamesoma upya mashtaka manane mbele ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Prosecution wameomba mahakama itoe hati ya kumkamata Hans Poppe kwa kuwa hakuwepo mahakamani wakati akijumuishwa katika kesi hiyo.

Hakimu Simba ameridhia ombi na kuelekeza hati itolewe na mahakama. Upelelezi wa kesi umekamilika.

Mtuhumiwa mwingine aliteongezwa katika kesi hiyo ni Franklin Lauwo ambaye anatuhumiwa kuitumia kampuni ya ukandarasi isiyosajiliwa ikapitishiwa pesa Dola 40,000 kama vile imelipwa kwa kazi wakati si kweli.

Haya ameyaeleza Leonard Swai, Mwanasheria wa TAKUKURU, wakati akiongeza washitakiwa na kusoma upya mashtaka.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!