MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope, ameongezwa katika kesi ya tuhuma za kughushi nyaraka na kujipatia fedha inayowakabili Rais wa klabu hiyo, Evans Aveva na Makamu wa wake, Godfrey Nyange ‘Kaburu’. Anaripoti Jabir Idrissa … (endelea).
Waendesha mashtaka leo wamesoma upya mashtaka manane mbele ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Prosecution wameomba mahakama itoe hati ya kumkamata Hans Poppe kwa kuwa hakuwepo mahakamani wakati akijumuishwa katika kesi hiyo.
Hakimu Simba ameridhia ombi na kuelekeza hati itolewe na mahakama. Upelelezi wa kesi umekamilika.
Mtuhumiwa mwingine aliteongezwa katika kesi hiyo ni Franklin Lauwo ambaye anatuhumiwa kuitumia kampuni ya ukandarasi isiyosajiliwa ikapitishiwa pesa Dola 40,000 kama vile imelipwa kwa kazi wakati si kweli.
Haya ameyaeleza Leonard Swai, Mwanasheria wa TAKUKURU, wakati akiongeza washitakiwa na kusoma upya mashtaka.
Leave a comment