Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee: Lowassa anavuja damu ya usaliti
Habari za SiasaTangulizi

Halima Mdee: Lowassa anavuja damu ya usaliti

Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu
Spread the love

HATUA ya Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema kurejea CCM imetajwa kwamba ni usaliti kwa waliomwamini na kumpigia kura kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe amesema, Lowassa ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema amelazimika kurejea CCM kutokana na kuelemewa na changamoto nyingi za kibiashara na kifamilia.

Mdee ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Machi 2019 kupitia andiko lake aliloandika katika ukurasa wake wa Twitter baada ya watu kuhoji ukimya wake kuhusu tukio la kuhama kwa Lowassa.

Aidha, Mdee ameeleza kuwa, anajua kwamba nafsi ya Lowassa inavuja damu ya usaliti kwa wananchi waliompigia kura za urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

“Natambua changamoto nyingi anazopitia za kifamilia na kibiashara, akalazimika kuomba po! sikuona haja ya kusema chochote nikiheshimu uamuzi wake.

“Najua nafsi yake inavuja damu ya usaliti kwa waliompa heshima na ‘kumrudishia uhai’(wananchi waliompigia kura nyingi sana)!,” ameandika Mdee.

Mdee amendika kuwa, hakuona haja ya kusema chochote kuhusu hatua ya Lowassa kurejea CCM, kwa sababu ameheshimu uamuzi wake.

Lowassa alirejea CCM tarehe 1 March 2019 akipokewa na Dk. Magufuli, Mwenyekiti wa CCM Taifa. Kwenye mapokezi hayo, Lowassa alizungumza maneno machache kwamba “nimerudi nyumbani.”

Pia alipokewa na Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally pamoja na baadhi ya viongozi wengine wa chama hicho katika ofisi ndogo za CCM zilizoko Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!