Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee atupwa ‘jela,’ Mbowe asamehewa
Habari za SiasaTangulizi

Halima Mdee atupwa ‘jela,’ Mbowe asamehewa

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe (kushoto) akiwa mbele ya Kamati ya Haki na Maadili ya Bunge
Spread the love

KAMATI ya Haki na Maadili ya Bunge imetoa adhabu kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kutohudhuria vikao vya Bunge la Bajeti vilivyobaki baada ya kumtia hatiani kwa kudharau mamlaka ya Spika na kutoa lugha ya matusi bungeni, anaandika Hamisi Mguta.

Uwamuzi huo umetekelezwa baada ya mjumbe wa kamati hiyo, Almasi Maige kuomba bunge lijadili na kutoa uamuzi.

Wakati huo huo, Kamati imetoa karipio kali kwa Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya, baada ya kukiri kosa la kudharau Bunge alilolifanya March 30, 2017.

Kamati hiyo pia imemsamehe, Freeman Mbowe kutokana na kosa la kutoa lugha isiyokuwa na staha kwa kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kwa sababu kosa lake lilikuwa la kwanza.

Mdee na Mbowe walikiri makosa kwenye kamati na kuomba radhi lakini kwakuwa Mdee ni kosa lake la pili kamati imechukua uwamuzi wa kumzuia kutohudhuria vikao hivyo vya Bunge la Bajeti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

error: Content is protected !!