Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee atupwa ‘jela,’ Mbowe asamehewa
Habari za SiasaTangulizi

Halima Mdee atupwa ‘jela,’ Mbowe asamehewa

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe (kushoto) akiwa mbele ya Kamati ya Haki na Maadili ya Bunge
Spread the love

KAMATI ya Haki na Maadili ya Bunge imetoa adhabu kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kutohudhuria vikao vya Bunge la Bajeti vilivyobaki baada ya kumtia hatiani kwa kudharau mamlaka ya Spika na kutoa lugha ya matusi bungeni, anaandika Hamisi Mguta.

Uwamuzi huo umetekelezwa baada ya mjumbe wa kamati hiyo, Almasi Maige kuomba bunge lijadili na kutoa uamuzi.

Wakati huo huo, Kamati imetoa karipio kali kwa Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya, baada ya kukiri kosa la kudharau Bunge alilolifanya March 30, 2017.

Kamati hiyo pia imemsamehe, Freeman Mbowe kutokana na kosa la kutoa lugha isiyokuwa na staha kwa kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kwa sababu kosa lake lilikuwa la kwanza.

Mdee na Mbowe walikiri makosa kwenye kamati na kuomba radhi lakini kwakuwa Mdee ni kosa lake la pili kamati imechukua uwamuzi wa kumzuia kutohudhuria vikao hivyo vya Bunge la Bajeti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!