Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee achukuliwa fomu BAWACHA
Habari za Siasa

Halima Mdee achukuliwa fomu BAWACHA

Spread the love

WAJUMBE wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA) wamemchukulia Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, fomu ya kugombea uenyekiti wa baraza hilo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Wajumbe hao wakiongozwa na Grace Kiwelu, Mwenyekiti wa BAWACHA mkoani Kilimanjaro wamechukua fomu hiyo leo tarehe 23 Novemba 2019, katika ofisi za Mbaraza ya Chadema, Kinondoni, Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kuchukua fomu hiyo, Kiwelu amesema wamechukua hatua hiyo, kwa kuwa BAWACHA linahitaji mchango wa Mdee, hasa katika kipindi hiki alichodai kwamba kina siasa za kibabe.

“Ni muhimu kuendelea kuwa naye kwa sababu bado tuna muhitaji, wale wanaotaka kuchukua fomu hatujawakataza chama chetu ni cha kidemokrasia. Na kila mtu ana mtu wake, na sisi wetu ni Halima. Kina mama tumeungana, tumekuchangia sh. 250,000,” amesema Kiwelu na kuongeza;

“Kwa siasa za sasa hivi za awamu ya tano zilivyo za kibabe, mwenyekiti wetu alikuwa mstari wa mbele ametuongoza na kutuwezesha kufika hapa, ni mwanamke jembe, suluru tunampenda. Mpaka sasa hatujamuona mwingine, tuliyemuona ni Halima ameonesha kwa vitendo ndio maana tumemuunga mkono.”

Halima amewashukuru wajumbe hao wa Bawacha kwa kumchukulia fomu, na kuahidi kwamba hatowaangusha kama atachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa BAWACHA.

“Miaka mitano iliyopita nililazimishwa kuchukua fomu, kwa kipindi kile sikudhani kama nilikuwa tayari, na kama mnakumbuka nililia sana kipindi kile.  Lakini sasa nimeshakuwa kamanda, silii kwa sababu mlinipa jukumu,kulisogeza baraza letu kutoka lilipokuwepo mpaka lilipofika sasa hivi, “ amesema Halima.

Halima anatarajia kurudisha fomu tarehe 28 Novemba mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!