Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Hakimu, Serikali wakwamisha kesi ya Kabendera
Habari MchanganyikoTangulizi

Hakimu, Serikali wakwamisha kesi ya Kabendera

Mwandishi Erick Kabendera akiwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imehairisha kesi namba 75 ya mwaka 2019 inayomkabili mwandishi wa kujitegemea wa habari za uchunguzi nchini, Erick Kabendera kutokana na upande wa Serikali kushindwa kukamilisha upelelezi. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Augustina Mmbando, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ameiomba mahakama hiyo kuahirisha shauri hilo kwa madai kuwa hakimu anayesikiliza shauri hilo Augustine Rwizile amepata dharura pia upande wao haujakamilisha upelelezi wa shauri hilo.

Jebra Kambole ambaye ni Wakili anayeongoza jopo la utetezi ameiomba mahakama hiyo kuwa upande wa Serikali uharakishe upelelezi kutokana na mshtakiwa kuwa hana dhamana.

Nje ya Mahakama hiyo, Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa amesema kuwa mashtaka yanayomkabili Kabendera yametokana na kazi zake anazozifanya, hivyo wadau wote wa habari na haki za binadamu nchini na ulimwenguni kwa ujumla wanapaswa kupaza sauti zao ili haki itendeke dhidi ya mwandishi huyo.

Aidha Olengurumwa ameviomba vyombo vinavyosimamia utoaji haki nchini ikiwemo vyombo vya uchunguzi kuchunguza kwanza kabla mshtakiwa hajafikishwa mahakamani ili kuepuka wimbi la mrundikano wa kesi nyingi mahakamani kutokana na uchunguzi kutokukamilika.

Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Agosti 30, 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB yakabidhi vifaa vya ujenzi, samani kwa shule ya msingi Sinyaulime, Chuo cha FDC Morogoro

Spread the loveBENKI ya NMB imekabidhi vifaa vya ujenzi kwa shule ya...

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

error: Content is protected !!