Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Hakimu, Serikali wakwamisha kesi ya Kabendera
Habari MchanganyikoTangulizi

Hakimu, Serikali wakwamisha kesi ya Kabendera

Mwandishi Erick Kabendera akiwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imehairisha kesi namba 75 ya mwaka 2019 inayomkabili mwandishi wa kujitegemea wa habari za uchunguzi nchini, Erick Kabendera kutokana na upande wa Serikali kushindwa kukamilisha upelelezi. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Augustina Mmbando, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ameiomba mahakama hiyo kuahirisha shauri hilo kwa madai kuwa hakimu anayesikiliza shauri hilo Augustine Rwizile amepata dharura pia upande wao haujakamilisha upelelezi wa shauri hilo.

Jebra Kambole ambaye ni Wakili anayeongoza jopo la utetezi ameiomba mahakama hiyo kuwa upande wa Serikali uharakishe upelelezi kutokana na mshtakiwa kuwa hana dhamana.

Nje ya Mahakama hiyo, Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa amesema kuwa mashtaka yanayomkabili Kabendera yametokana na kazi zake anazozifanya, hivyo wadau wote wa habari na haki za binadamu nchini na ulimwenguni kwa ujumla wanapaswa kupaza sauti zao ili haki itendeke dhidi ya mwandishi huyo.

Aidha Olengurumwa ameviomba vyombo vinavyosimamia utoaji haki nchini ikiwemo vyombo vya uchunguzi kuchunguza kwanza kabla mshtakiwa hajafikishwa mahakamani ili kuepuka wimbi la mrundikano wa kesi nyingi mahakamani kutokana na uchunguzi kutokukamilika.

Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Agosti 30, 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!