Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Hakimu agoma kumpa dhamana mtuhumiwa sugu wa bangi
Habari Mchanganyiko

Hakimu agoma kumpa dhamana mtuhumiwa sugu wa bangi

Spread the love

MOHAMED Hamis, mtuhumiwa aliyekutwa na bangi yenye uzito wa kilo 0.57 amekataliwa dhamana kutokana na kuwa ‘mzoefu’ kukamwata na makossa ya namna hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika Mahakama ya Mkazi Kinondoni jijini Dar es Salaam, Hakimu Bonifasi Lihamwike ameeleza kuwa, hatompa dhamana Mohamed (24) kwa kuwa, tayari amefikishwa kwenye mahakama hiyo mara nne kwa kosa moja.

Akisomewa shitaka hilo mbele ya Hakimu Bonifasi Lihamwike, Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Veronika Mtafia alidai kuwa Januari 10, mwaka huu eneo la Sinza Kwa Mori, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam mshitakiwa alikutwa na kiasi hicho cha dawa za kulevya huku akijua ni kinyume cha sheria.

Mshitakiwa alikana kutenda kosa hilo huku upande wa Jamhuri ukisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba tarehe ya kutajwa tena.

Hata hivyo, Hakimu Lihamwike amesema, kutokana na mtuhumiwa kurudishwa mara nne mahakamani kwa wakati tofauti kwa tuhuma ya kukutwa na dawa za kulevya, mahakama imeamua kutompa dhamana kwa kesi hiyo mpaka hukumu itakapotolewa.

Hemed amerudishwa rumande hadi kesi yake itakaposomwa tena tarehe 25 Machi 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!