Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Guinea-Bissau: Wengi walikufa baada ya jaribio la mapinduzi, Rais anasema
Kimataifa

Guinea-Bissau: Wengi walikufa baada ya jaribio la mapinduzi, Rais anasema

Spread the love

 

MAPINDUZI yameripotiwa katika nchi ya Afrika Magharibi ya Guinea-Bissau, yamesababisha vifo vya maafisa kadhaa wa vikosi vya usalama, rais wake anasema. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Umaro Cissoko Embaló alisema, hali imedhibitiwa nakuitaja kuwa “kushindwa kwa mashambulizi dhidi ya demokrasia.”

Makabiliano ya risasi yalizuka karibu na jengo la serikali Jumanne ya tarehe 1 Februari 2022 katika mji mkuu wa Bissau ambapo rais aliripotiwa kuhuduria mkutano wa Baraza la Mawaziri.

Watu wasiojulikana waliokuwa na silaha nzito walishambulia Ikulu ya serikali wakati Rais Embaló alipokuwa akikutana na Waziri Mkuu, Nuno Gomes Nabiam, kulingana na ripoti kutoka eneo la tukio.

Shirika la utangazaji la BBC, limenukuu vyanzo mbalimbali vya taarifa vikisema, wanaume waliokuwa wamejihami kwa bundukiwa wakiwa wamevalia nguzo za nyumbani, walimpiga risasi na kumuua afisa wa polisi.

Umaro Sissoco Embaló, alichaguliwa kuwa rais mwaka 2019.

Viongozi wa Kanda ya Afrika Magharibi walielezea tukio hilo kama jaribio la mapinduzi na kuwataka wanajeshi kurejea kwenye kambi.

Lakini kilichotokea bado hakijabainika. Bado haijajulikana mtu aliyejihami ni nani na rais hakutoa idadi kamili ya waliouawa.

Nchi hiyo masikini na koloni la zamani na Ureno, imeshuhudia mapinduzi tisa au majaribio ya mapinduzi tangu mwaka 1980.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!