Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Guardiola, Solskjaer kwenye vita kocha bora England
Michezo

Guardiola, Solskjaer kwenye vita kocha bora England

Spread the love

 

MAKOCHA Pep Guardiolla wa Manchester City na Ole Gunner Solskjaer wa Manchester United wamejuimishwa kwenye orodha ya makocha watano kuwania tuzo ya kocha bora wa Ligi Kuu nchini England kwa msimu wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Orodha hiyo imetolewa hii leo ambapo wadau mbalimbali watapata nafasi ya kupiga kura ya kumchagua kocha bora kwa msimu uliomalizika.

David Moyes, kocha wa Westham United

Guardiola amejuimuishwa kwenye kikosi hiko mara baada ya kuiongoza klabu yake ya Manchester City kutwaa taji la Ligi Kuu nchini humo kwa mara ya tatu Katika kipindi cha miaka mitano aliyokaa hapo.

Kwa upande wa kocha wa Manchester United Ole Gunner Solskjaer yeye ameingia kwenye kinyang’anyiro hiko mara baada kuiongoza klabu ya Manchester United kumaliza nafasi ya pili kwenye msimamo.

Marcelo Bielsa mocha wa Leeds United

Makocha hayo wawili walifanikiwa pia kuongoza timu zao kwenye fainali mbili kubwa barani Ulaya kwenye ngazi ya klabu na wote walipoteza.

Guardiola aliingai fainali ya michuano ya kombe la Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya na kupoteza mchezo huo kwa bao 1-0, dhidi ya Chelsea, Solskjaer akiwa na kikosi cha Manchester United walipoteza mchezo wa fainali ya Europa kwa mikwaju ya penati dhidi ya Villarreal.

Brendan Rodgers kocha wa Leicester City

Makocha wengine waliongia kwenye kinyang’anyiro hiko ni Marcelo Bielsa wa Leeds United, David Moyes wa West Ham United pamoja na Branden Rodgers anayekinoa kikosi cha Leceister City.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!