BABA mzazi wa mfanyabiashara maarufu na mfadhiri wa klabu ya Yanga, Ghalib Said Mohammed (GSM), mzee Said Mohamed amefariki Dunia leo Jumanne tarehe 1 Machi 2021, Masaki jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Taarifa za kifo hiko zilitolewa leo asubuhi na Mkurugenzi wa uwekezaji wa kampuni ya GSM, Mhandisi Hersi Said kupitia kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mazishi ya Mzee Said Mohammed yatafanyika hii leo majira ya saa 10 jioni kwenye makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam na swala itaswaliwa kwenye msikiti wa Maamur uliopo Upanga.
Mara baada ya kutokea msiba huo, watu mbalimbali maarufu kupitia mitandao ya kijamii walitoa pole kwa familia ya mfanyabiashara huyo, ambaye hivi karibuni alikuwa nchini Dubai.
Kwa upande wa klabu ya Yanga, nao walitoa salamu zao za pole kwa familia ya mfadhiri wao Ghalib Said kwa msiba huo, kupitia taarifa rasmi waliyoitoa hivi punde.
Leave a comment