Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo GSM wamkaribisha Manji Yanga
Michezo

GSM wamkaribisha Manji Yanga

Yusuf Manji
Spread the love

 

MARA baada ya kurejea nchini kwa mfanya biashara Yusuf Manji na kuibuka kwa hisia kali za mashabiki wa klabu ya Yanga kutaka arejee ndani ya klabu hiyo, wafadhiri wa timu hiyo kwa sasa kampuni ya Gsm wamemkaribisha mwenyekiti huyo wa zamani kwa mikono miwili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Manji alirudi nchini siku tatu zilizopita mara baada ya kuondoka nchini toka mwaka 2018 kutokana na matztizo yake binafsi.

Akiongea na chombo kimoja cha habari Mkurugezni wa uwekezaji wa kampuni ya Gsm ambao ni wadhamini wa klabu ya Yanga, Mhandisi hersi Saidi amesekuwa wanamkaribisha mwenyekiti huyo kwa mikono miwili kutokana na klabu hiyo kuwa na mahitaji mengi kwa sasa.

“Hii itakuwa Baraka kubwa kwetu kama Gsm, kwa sababu ilikuwa tiukiita watu kuisapoti timu, Yanga inamahitaji mengi sana kwa kuwa mapato na matumizi ya klabu hayafaniani ndio maana sisi tuliingia kusapoti hii, akitokea mtu tutafurahi sana.” Alisema Hersi

Mhandisi Hersi Said, Mkurugezni wa uwekezaji Gsm

Aidha kiongozi huyo aliongezea kuwa kama akitokea mtu anataka kuongeza nguvu ndani ya Yanga watampokea kwa mikono miwili.

“Akitokea mtu akisema Gsm nataka niongeze nguvu ya kuisapoti Yanga tutampokea kwa mikono miwili.” Aliongezea kiongozi huyo

Mukoko Tonombe mchezaji wa klabu ya Yanga

Manji ambaye alikuwa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga toka mwaka 2012 alipata mafanikio makubwa ikiwemo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mara tatu mfululizo kuanzia msimu wa 2014 mpaka 2017.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!