Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Green Mile yamgomea Kigwangalla
Habari Mchanganyiko

Green Mile yamgomea Kigwangalla

Spread the love

KAMPUNI ya Uwindaji ya Green Mile imeendelea kuvutana na Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla, kwa kile walichodai kuwa wataendelea na shughuli zao. Anaripotia Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Said Mndeme, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, amesema kuwa hakuna taarifa yoyote ya serikali iliyowafikia kuhusu kufutwa kwa kitalu chao.

“Kuna taarifa zinazagaa kwenye mitandao ya kijamii zinazomuhusisha Dk. Kigwangalla kuwa amefuta umiliki wa kitalu cha uwindaji  wa kitalii cha Lake Natron East, kinachomilikiwa na kampuni ya Green Mile Safari.

“Kampuni inazitafsiri taarifa hizo kuwa ni muendelezo wa mkakati wa kuichafua kampuni ya kuiharibia biashara yake. Kampuni yetu haina taarifa yoyote kutoka Serikalini,” amesema Mndeme.

Amesema kuwa shughuli za uwindaji wa kitalii kwenye kitalu hiko zitaendelea kama kawaida.

Amesema kuwa hawaitambui taarifa hiyo kwa sababu ya kukiuka fungu la 38 la sheria ya wanyamapori ya mwaka 2009.

Amedai kuwa baadhi ya watendaji serikalini wamekuwa wakiwakwamisha kwa maslahi yao binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!