Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Gonjwa hili, Ukimwi haugusi
Afya

Gonjwa hili, Ukimwi haugusi

Spread the love

UPUNGUFU wa Kinga Mwilini (Ukimwi) ndio unaoonekana kuwa tishio lakini Ugonjwa wa Homa ya Ini unatajwa kuuwa Ukimwi na hata Kifua Kikuu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Prof. Muhammad Bakari wakati akihutubia wananchi katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Homa ya Ini Duniani leo Julai 28, 2018.

Prof. Bakari ameeleza kuwa, takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) kupitia ripoti ya Homa ya Ini ya mwaka 2017 zinaonesha kuwa, mwaka 2015 kulikuwa na vifo milioni 1.34 kutokana na Homa ya Ini ambavyo vilikuwa sawa na vifo vitokanavyo na Kifua Kikuu na zaidi ya vile vitokanavyo na ugonjwa wa UKIMWI ambavyo vilikuwa milioni 1.1.

Kwa hapa nchini, amesema takwimu kutokana na tafiti zilizopo zinaonesha uwepo wa maambukizi ya virusi vya Homa ya Ini aina ya B na C, na kwamba

kati ya wachangiaji damu 200,000 kwa mwaka 2016, asilimia 6 ambayo sawa na takriban watu 12,000 walikuwa na maambukizi ya Homa ya Ini aina ya B.

Wakati mwaka 2017, kati ya wachangiaji damu 233,953, 4.9% takriban watu 11,417 walikuwa na maambukizi ya Homa ya Ini aina ya B na 0.5% takriban watu 1,170 walikuwa na maambukizi ya Homa ya Ini aina ya C.

“ Aidha, utafiti mahsusi ujulikanao kama “THIS”, ulioratibiwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu, umeonesha kuwa maambukizi ya Homa ya Ini aina ya B ni 4.3% miongoni mwa watanzania wenye umri kati ya miaka 15-49, kwa mwaka 2017. Vilevile, miongoni mwa wanajamii, Homa ya Ini inayosababishwa na virusi aina ya C inakadiriwa kuwepo kwa 2%,” amesema na kuongeza.

“Wananchi wa Tanzania na Afrika Mashariki wapo katika hatari ya kupata maambukizi ya Homa ya Ini, hususan aina ya B na C, kutokana na kuwa njia za maambukizi ya Virusi hivi hufanana na zile za maambukizi ya VVU.”

Prof. Bakari amesema serikali ianendelea kuimarisha mikakati ya kuweza kudhibiti ugonjwa huo kwa kuongeza kuongeza juhudi za kutekeleza Mpango Mkakati wa kwanza wa Dunia wa Homa ya Ini (Global Health Sector Strategy on Viral Hepatitis) kwa mwaka 2016-2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!