Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Gomes, Bocco wapeta tuzo mwezi Juni
Michezo

Gomes, Bocco wapeta tuzo mwezi Juni

John Bocco mshambuliaji wa Simba
Spread the love

 

KOCHA wa klabu ya Simba, Didier Gomes pamoja na mshambuliaji wa klabu hiyo John Bocco wameshinda tuzo, mwezi Juni kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Bocco ambaye pia ni nahodha wa kikosi hiko, ameshinda tuzo hiyo mara baada ya kufanya vizuri kwenye michezo ya mwezi Juni.

Katika mwezi Juni Bocco amecheza jumla ya michezo mitatu na kupachika mabao matatu ambapo timu yake iliibuka na ushindi katika michezo hiyo.

Kwenye kinyang’anyiro hiko, Bocco amewashinda wachezaji Feisal Salum wa Yanga, pamoja Iddi Suleiman anayekipiga na Azam FC.

Didier Gomes kocha wa Simba

Hii itakuwa mara ya pili kwa Bocco kutwaa tuzo hiyo, mara ya kwanza kwa msimu huu ilikuwa mwezi Novemba, mwaka jana.

Kwa upande wa kocha Gomes yeye alifanikiwa kunyakuwa tuzo hiyo, mara baada ya kuikngoza Simba kushinda michezo yote mitatu ya mwezi Juni, ambapo aliibuka na ushindi wa mabao 3-0, dhidi ya Ruvu Shooting, pia aliibuka na ushindi wa bao1-0, mbele ya Polisi Tanzania na kisha kuichakaza Mbeya City mabao 4-0.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!