Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya GGML yaadhimisha siku ya mazingira duniani kwa kutoa elimu kuhusu taka za plastiki
Afya

GGML yaadhimisha siku ya mazingira duniani kwa kutoa elimu kuhusu taka za plastiki

Spread the love

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML) ambayo ni moja ya migodi maarufu ya AngloGold Ashanti nchini Tanzania, imeadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kutoa elimu kuhusu aina mbalimbali za taka za plastiki na ugawaji wa vifaa vya kuhifadhi taka kwa lengo la kuwawezesha wananchi kutenganisha ipasavyo taka za plastiki. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Siku ya Mazingira Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Juni, ni tukio muhimu la kimataifa lililoandaliwa na Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa, na mwaka huu kauli mbiu ni “Tokomeza uchafuzi wa mazingira unaotokana na taka za plastiki”.

Afisa Uhusiano wa GGML, Dafroza Manyanda (kushoto) akikabidhi vifaa vya usafi kwa Mwenyekiti wa mtaa wa Uwanja uliopo katika Halmashauri ya Geita, Enos Cherehani.

Kauli mbiu hiyo inalenga kusisitiza kwamba taka za plastiki ni tatizo la kimataifa ambalo linatishia mazingira, wanyamapori na afya ya binadamu.

Akizungumza katika tukio hilo lililofanyika katika mji wa Geita kwa kuwashirikisha wafanyakazi wa GGML na mamlaka za mitaa, Meneja Mazingira wa Mgodi huo Yusuph Mhando alisema GGML inafahamu kuwa uchimbaji madini una athari ya moja kwa moja kwa mazingira kwani rasilimali za ardhi na maji zinahitaji kuendelezwa.

Alisema kampuni hiyo imejidhatiti katika utunzaji wa mazingira na imechukua hatua mbalimbali ili kupunguza mwelekeo wake wa mazingira na kuongeza mchango wake chanya kwa jamii zinazozunguka Geita.

“Moja ya hatua hizo ni usimamizi wa taka za plastiki kutoka vyanzo mbalimbali kama vile vifungashio, vifaa vya kujikinga, chupa za maji na vyombo vya chakula. Kampuni pia inatoa mafunzo kwa wafanyakazi na wakandarasi wote kutenganisha na kutupa aina tofauti za taka kwa kutumia mapipa yenye alama za rangi na lebo. Wafanyakazi wote na wakandarasi hupokea mafunzo ya mazingira ili kuhakikisha uzingatiaji wa sera na taratibu za usimamizi wa taka.

Alisema GGML inafanya kazi kwa pamoja ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kupunguza, kutumia tena na kuchakata plastiki.

Afisa Mawasiliano Mwandamizi kutoka GGML, Laurian Pima akizungumza na wakazi wa mtaa wa Uwanja katika Halmashauri ya Geita na kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kutenganisha taka za plastiki ili kulinda mazingira ikiwa ni muendelezo wa jitihada za kampuni hiyo katika kuhifadhi mazingira.

“Tunajivunia kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani na kushirikisha jamii zinazozunguka mgodi katika kuendeleza desturi nyetu ya kulinda na kuhifadhi mazingira yetu, tunaamini kwa kuwaelimisha na kuwawezesha wananchi kutenganisha ipasavyo taka za plastiki tunaweza kuleta mabadiliko chanya katika vita dhidi ya uchafuzi wa plastiki.

“Pia tunahimiza kila mtu kuzingatia kanuni ya 3Rs: Punguza, Tumia Tena na Usafishaji plastiki kila inapowezekana,” alisema.

GGML inachukua jukumu lake la kupunguza athari zake za mazingira kwa umakini na imejitolea kuwajibika kwa usimamizi wa mazingira.

Aliongeza kuwa mgodi huo umekuwa ukifanya kazi nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 20 na ni miongoni mwa walipakodi wakubwa na wanaokidhi viwango vinavyozingatia sheria nchini. GGML inaajiri zaidi ya watu 5,000 moja kwa moja na kupitia wakandarasi na takriban asilimia 98 kati yao ni raia wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!