KAMPUNI ya GF Trucks & Equipmentís imepanga kuanza kuwakopesha vitendea kazi wakandarasi ili kuhakikisha wakandarasi wadogo na wakati. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Lengo ni kuwakomboa na hali mbaya ya kuchelewesha miradi mbalimbali wanayopatiwa.
Hayo yamesemwa leo Alhamisi tarehe 12 Mei 2022 jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Kampuni ya Uuzaji wa Magari (trucks) na Mitambo ya Kutengenezea Barabara wa GF Trucks & Equipmentís Ltd, Salman Karmal katika mkutano wa Bodi ya Wakandarasi Tanzania.
Karmal amewataka wakandarasi na wahandisi nchini kununa magari na mitambo katika kampuni hiyo kwani wanautaratibu mzuri wa kuwakopesha wakandarasi wadogo na wakati ambao wana miradi tayari.
Amesema GF wanakitengo maalumu kwa kushirikiana na taasisi za kibenki ili kumwezesha mkandarasi kupata mitambo na magari kwa masharti nafuu.
Kampuni hiyo inayojishungulisha na uuzaji wa Magari ya FAW, HONG YANG na mitambo aina ya XCMG.
Mmoja wa wanufaika wa mpango huo wa kampuni hiyo ambaye amefaidika na huduma hiyo ya kukopeshwa vitendea kazi, Mhandisi Baraka Emanueli amesema, kupitia kampuni hiyo walianza na Tipper moja na sasa wanamiliki magari matatu walioanza kukopa miaka mitatu iliyopita.
Amesema wamefanikiwa kulipa na hatimaye kwa sasa wamechukua mashine ya XCMG hivyo utaratibu huo umewanufaisha wao ambapo wanapata zabuni za kuchukua makaa ya mawe ambayo awali hawakuwa na uwezo.
Leave a comment