Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Gazeti la MwanaHALISI lawakutanisha Waziri Bashungwa, Kubenea
Habari MchanganyikoTangulizi

Gazeti la MwanaHALISI lawakutanisha Waziri Bashungwa, Kubenea

Spread the love

 

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa, amekutana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali Halisi Publishers, Saed Kubenea kuzungumzia tasnia hiyo ya habari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kubenea, aliyewahi kuwa mbunge wa Ubungo 2015-2020, alifika ofisini kwa Bashungwa, jana Ijumaa tarehe 9 Aprili 2021, jijini Dodoma, akiitikia wito wa waziri huyo, alioutoa hivi karibuni.

Ni baada ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuagiza kufunguliwa kwa vyombo vya habari vilivyofungiwa huku akisisitiza lazima, vizingatie sheria na kanuni za uendeshaji wa tasnia hiyo nchini.

Waziri Bashungwa, aliagiza wamiliki wa magazeti ambayo yalifungiwa kufika ofisini kwake ili kujadiliana na kuona jinsi ya kumaliza changamoto zilizokuwapo.

Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo baada ya majadiliano kati ya waziri na Kubenea ambaye kampuni yake inachapisha Gazeti la MwanaHALISI na Mseto yaliyofungiwa, imesema Bashungwa ametoa wito kwa wadau wa tasnia ya habari kuunga mkono dhamira ya Rais Samia kuona haki ya uhuru wa habari inaendana na wajibu na uzingatiaji sheria, kanuni na misingi ya taaluma ya habari.

Gazeti la MwanaHALISI lilifungiwa na Serikali, Septemba 2017 kwa miaka miwili. Lilifungua kesi ndani na katika Mahakama ya Kuu ya Tanzania na kushinda kesi, wakati gazeti Mseto lilifungua kesi Mahakama ya Afrika Mashariki na kushinda pia, ila hayakufanikiwa kurejea mtaani mpaka sasa kutokana na kutopata leseni ya uchapishaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!